Utangulizi na Muhtasari
Huduma jumuishi za kifedha huchangia katika ujumuishi wa kifedha katika sekta ya fedha, kwa mtu mmoja mmoja na biashara kufikiwa na kutumia bidhaa na huduma mbalimbali za kifedha zenye ubora wa hali ya juu kwa gharama nafuu ili kuboresha ustawi wa kifedha na kipato.
Huduma jumuishi za kifedha na ustawi huiwezesha Benki Kuu ya Tanzania kutimiza majukumu yake ya kusimamia utekelezaji wa sera ya fedha, kuboresha imani na uthabiti wa sekta ya fedha yenye hali nzuri ya kuwezesha maendeleo endelevu ya uchumi wa Taifa letu.
Benki Kuu kama Sekretarieti ya Baraza la Taifa la Huduma Jumuishi za Kifedha, inatekeleza na kuratibu mikakati ya huduma jumuishi za kifedha kama ilivyoainishwa kwenye Mpango Mkakati wa Huduma Jumuishi za Kifedha kupitia ushirikiano na ubia kati ya sekta ya umma na binafsi. Vilevile, Benki Kuu ina jukumu la kuwalinda walaji wa bidhaa na huduma za kifedha kwa taasisi zote inazozisimamia.
Hivi karibuni, Tanzania imepitia mabadiliko makubwa kwenye sekta ya fedha ya kichochewa na kasi ya ongezeko la matumizi ya teknolojia katika kuzalisha na kusambaza bidhaa na huduma za kifedha. Mabadiliko haya, yanazidi kuifanya Tanzania kubaki kuwa mstari wa mbele ukanda huu kwenye masuala ya huduma jumuishi za kifedha. Pamoja na haya, bado upo uwiano usiosawia katika upatikanaji na matumizi ya huduma rasmi za kifedha nchi nzima kwa rika la watu wa wazima.
Ili kukabiliana na changamoto hizi, matumizi ya teknolojia ya kidigitali katika utuoaji wa huduma za fedha ili kuwa na wigo mpana wa kuyafikia makundi yasiyo na huduma, au yenye uhaba wa huduma rasmi za kifedha nchini. Katika kutekeleza majukumu haya, pamoja na mambo mengine, ilisaidia kupanua wigo wa upatikanaji na matumizi ya huduma rasmi za kifedha nchini. Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti ya FinScope 2023, kiwango cha upatikanaji na matumizi ya huduma rasmi za kifedha kiliongezeka hadi kufikia 89% na 76% mwaka 2023 toka 86% na 65%, mtawalia. Hata hivyo, pamoja na mafaniko haya, kiwango cha watu walio nje ya huduma rasmi za kifedha bado kipo juu kwa baadhi ya makundi yakiwemo ya wakaazi wa vijijini, wakulima wadogo, vijana na wanawake.
Uthabiti wa sekta ya fedha ni hali ambayo mfumo wa kifedha unaojumuisha taasisi za kifedha, masoko ya kifedha na miundombinu ya masoko ya kifedha una uwezo wa kuhimili mishtuko na mkusanyiko wa kutokuwiana kwa kifedha, huku ukiendelea kutoa huduma muhimu za kifedha kwa kaya, biashara na uchumi kwa ujumla.
Mfumo wa kifedha ulio imara na unaofanya kazi kwa ufanisi huchangia ukuaji endelevu wa uchumi kwa kuhakikisha kuwa upatanishi wa kifedha unafanyika kwa ufanisi na bila ya usumbufu mkubwa. Mfumo huo huwezesha kaya na biashara kuweka akiba, kukopa, kuwekeza, kujikinga dhidi ya hatari, kufanya malipo, kusimamia hatari na kupanga kwa ajili ya siku zijazo kwa kujiamini.
Utulivu wa kifedha si tu kutokuwepo kwa hali ya kuyumba kwa mfumo wa kifedha. Unahitaji uwepo wa mfumo wa kifedha ulio imara, wenye ustahimilivu na wenye uwezo wa kufyonza mishtuko hasi huku ukiendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi, hata wakati wa vipindi vya msongo wa kifedha.
Mifumo ya kifedha imeunganishwa kwa kiwango kikubwa, na kushindwa au matatizo yanayoikumba taasisi ya kifedha, soko la kifedha au mfumo wa malipo yanaweza kusambaa kwa haraka katika maeneo mengine ya mfumo wa kifedha. Kudumisha utulivu wa kifedha ni moja ya majukumu muhimu ya Benki Kuu na mamlaka za usimamizi wa sekta ya fedha. Hili linahusisha utambuzi, tathmini na ufuatiliaji endelevu wa udhaifu na hatari za kimfumo ndani ya mfumo wa kifedha, pamoja na utekelezaji wa hatua stahiki za kisera ili kupunguza hatari hizo na kuimarisha ustahimilivu wa sekta ya fedha.