Kuhakikisha kuwa kuna mifumo ya malipo ya taifa ya kuaminika, salama, rahisi, yenye gharama nafuu na iliyounganishwa ili kukidhi mahitaji ya kiuchumi.
Kuboresha uwezo wa nchi kusimamia uchumi mdogo mdogo kwa kutoa taarifa sahihi na kwa wakati juu ya hisa na mzunguko wa fedha.
Kuwezesha ubadilishanaji na makubaliano ya kifedha na dhamana ili kupunguza fedha iliyo kwenye mzunguko na kuboresha ufanisi katika mzunguko na upelekaji wa fedha.
Kutanua wigo katika mifumo ya malipo kwa kuzingatia maendeleo ya teknolojia kutegemeana na mahitaji ya watumiaji.
Kuhakikisha uwepo wa mifumo ya kisheria na kitaasisi iliyo imara na yenye ufanisi inayoweza kusimamia mifumo ya malipo.
Kazi ya Benki Kuu katika Mifumo ya Malipo ya Taifa
Kutengeneza sera za mifumo ya malipo ya Taifa kulingana na mahitaji mbalimbali ya sekta zote nchini.
Kutambua majukumu ya msingi ya mifumo ya malipo ambayo wadau mbalimbali, ikiwamo Benki Kuu ya Tanzania, wanatakiwa kuyafanya katika kuendeleza, kutekeleza, kuendesha, na kusimamia mifumo ya malipo ya Tanzania.
Kuishauri Serikali na jamii juu ya Mambo yanayohusu mifumo mbalimbali ya Malipo.
Kuratibu, kuoanisha na kuridhia mchakato wa viwango na mikakati ya pamoja ya mifumo ya malipo katika ngazi ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa.
Kuiwakilisha nchi katika majukwaa ya Kitaifa na Kimataifa kuhusu Mifumo ya Malipo.
Kuwasiliana moja kwa moja au kupitia Kamati za Mifumo ya Malipo ya Taifa na wadau na vyombo vya kimataifa kama vile BIS, Benki ya Dunia, SADC, EAC, na washauri wengine.
Kuhakikisha kwamba Mifumo ya Malipo iliyopo ikiwamo Miundo na Sheria inasimamiwa, kudumishwa na kuzingatiwa ipasavyo.
Kutoa leseni na vibali vya kutoa huduma za mifumo ya malipo kulingana na Sheria ya Mifumo ya Malipo ya Taifa
Kuhakiki na kushauri juu ya huduma mpya za mifumo ya malipo na vile vile kutengeneza miongozo juu ya matumizi na uanzishwaji wa huduma hizo.
Kuandaa kampeni na vipindi mbalimbali vya uhamasishaji, kuhusu mifumo yote mipya ya malipo