Wigo wa Sera ya Fedha
Benki Kuu ya Tanzania huandaa na kutekeleza Sera ya Fedha ikiwa kwa lengo la kuhakikisha utulivu wa bei nchini ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuhakikisha uimara wa sekta ya fedha. Hata hiyo ni vyema ikafahamika kuwa, kwa wakati mwingine, mfumuko wa bei wa jumla huathiriwa na mitikisiko ya upande wa ugavi (supply side shocks) ambazo ni nje ya wigo wa sera ya fedha. Vilevile, sera ya fedha ya kuongeza ukwasi kwa muda mfupi ndiyo inayoweza kuchochea ukuaji wa uchumi kutokana na kutobadilika kwa bei za bidhaa (perceived rigidity of prices). Hivyo, utekelezaji wa sera ya fedha ya kuongeza ukwasi kwa kipindi kirefu hausababishi kuongezeka kwa ukuaji wa uchumi isipokuwa hupelekea kuongezeka kwa bei za bidhaa.