Jukumu la Benki Kuu

Jukumu la msingi la Benki Kuu ya Tanzania ni kuandaa na kutekeleza sera ya fedha inayolenga kudhibiti mfumuko wa bei na kujenga mfumo wa fedha ulio imara na unaofaa kwa ukuaji endelevu wa uchumi wa taifa.

Majukumu mengine ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Kutoa sarafu ya nchi ambayo ni Shilingi ya Tanzania
  • Kusimamia na kudhibiti mabenki na taasisi za fedha
  • Kusimamia na kudhibiti mifumo ya malipo nchini.
  • Kuhifadhi akiba ya nchi ikiwemo fedha za kigeni
  • Benki ya Serikali
  • Benki ya Mabenki; na
  • Kutoa ushauri juu ya masuala ya uchumi na fedha kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar